Wandugu
wapenzi,
1.
Katika mkusanyo wetu uliofanyika pa Kinshasa
tarehe 10 mpaka 15 febrario 2003, sisi Maakina, Kardinali, Arkiaskofu
na Askofu wanamemba wa Kamati ya Baraza Kuu la Maaskofu wa Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo, tukiyafanya yetu maneno yake Bwana
: “ Nimeiona, nimeiona taabu ya taifa langu” (Kut. 3,7), tunatoa
kwa wakristu katoliki na watu wote wa mapenzi mema ujumbe huu :
2.
Kufwatana na kazi ya uchungaji tuliyoamnishwa na katika uaminifu
kwa mapokeo ya kinabii katika Eklezia, hatuchoki kulalamika juu ya hali
mbaya linamoishi taifa la Kongo. Mbele ya mwanzo wa Mzozo wa wakongomani
kati yao, tuliona kama mzozo huo ulikuwa
wa lazima sana na hakukua njia
ingine.
Tuna uchungu mno moyoni kwa kuona ya kwamba Mzozo huu haufikii
ukomo wake. Mkataba uliyofanyika pale Sun City haikushikwa, hakuna kitu
kilichotendeka na umeongeza tu fujo. Zaidi ya hayo imechongewa vilema
vingi mpaka tufikie kwenyi Mkataba mwingine uitwao wa jumla.
Mkataba wa jumla
3.
Wakongomani walipokea Mkataba wa Pretoria III na kitulizo pia na
masito. Lakini tangu sahihi iliwekwa juu ya Mkataba huo, wasiwasi la taifa
la Kongo imeendelea na kuongezeka pia. Mwisho wa vita unakawia kufika.
Mkataba uliofanyiwa na kelele sana ulimwenguni kote hauheshimiwi. Lakini
mapambano ya vita yameamka tena katika pande mbalimbali za Kongo na kuleta
tena taabu zaidi. Maovu yanatendewa juu ya rahiya na juu ya wafungwa kwa
sababu ya vita. Wapiganaji vita wanahepahepa na kuzidisha visingizio ili
vita idumu. Mpito hauanzi kamwe. Taabu la rahiya haivumiliki tena.
4.
Kwa kuona hali hiyo isiyoweza kuvumiliwa tena, Sisi, Wachungaji wa
taifa la Mungu la hapa Kongo, tunasema : « mno ni mno ! ».
Tunawastaki na nguvu yetu yote Washindani kwa ajili ya ujanja wao, kwa
ajili ya kutoshtuka kwao mbele ya taabu ya rahiya, pia kwa ajili ya ukaidi wao
wa kufululiza vita.
Ukosefu
wa utashi wa siasa na mapendo ya inchi
5.
Ukawio na mambo ya kuzungukana kwa kuheshimu Mkataba wa jumla
vinahakikisha ukosefu wa utashi ao moyo wa siasa na mapendo ya inchi dani
ya wanaopigana Kongoni. Ngambo zote mbili kuna watu, wachache lakini,
wasio na adibisho kamili la siasa wanaoshika taifa nzima kama mateka ;
wanatia sahihi juu ya Mikataba, lakini hawafanyi nguvu kwa kuiheshimu.
Heshima la ahadi ni fazila wanayozarau.
6.
Kwao, hakuna maambatano kati ya neno na tendo ; hii inashuhudia wazi ukosefu wa ajabu
wa roho ao wa utashi ya kuitumikia taifa. Wanafunga na kuvunja bila shida
maagano wakifwata tu mapenzi na faida yao peke. Wanasema kitu, lakini
wanafanya umbalimbali na yale wanayotoka kusema ; wanaimba amani,
lakini wanatumikia vita.
7.
Ukosefu huo wa utashi wa siasa umezaa Mkataba usio
na shurtisho wazi la kuacha vita katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
upandeni wa waliotia sahihi. Anayesoma Mkataba huo, anashangaa
kuona kama hakuna tangazo lolote la kukomesha vita. Lakini Mkataba
huo unaonekana kuwa makubaliano tu kati ya wapigana vita, na tuzo kwa
wasimamiao vita. Mgawanyo wa uwezo wa kuongoza una na fasi kubwa, kama
vile uwezo huo ungalikua ukomo kwa wao wenyewe. Ndiyo sababu mabishano
yamefikia kwenyi Mkataba unaoweka fasi ya kwanza wazo la kuchukua uwezo
kwa silaha. Lakini rahiya imeishakataa njia hiyo ya silaha.
Maana, inaonekana kama haikubaliwe kuendelea kutenda kufwatana na wazo la
vita kwani haisaidie kwa maendeleo ya nchi wala kwa kusimika kidemokrasia,
ginsi twajuwavyo.
8.
Watu wa siasa wa nchi yetu hawaonyeshi hata kidogo alama ya mapendo
ya nchi. Wakishurulika na faida yao wenyewe, wanafanya siasa kuwa chombo
cha pato, hawashuruliki kamwe kutafuta hali nzuri ya rahiya wala
kidemokrasia. Vyote ni wazi ; vitendo vya haya walivyotenda huko Sun
City, migawanyo
kati yao, shuruli kwa kupata fasi pamoja na magombezi juu ya kuwa
mkubwa zaidi ao wa kwanza, hayo yote ni mazoezi yao katika siasa. Watu wa
siasa wa kwetu wanashindwa kujisahau na kupigania mbele mafaa makuu ya
nchi ; wanafurahiwa tu kutia vikwazo vya kila namna ili vita iendelee
katika inchi ya JKK. Hali ya taabu
ya rahiya haiwastushe. Hawahangaiki hata kidogo kwa kutafuta kweli
kidemokrasia. Tangu hapo, haishangaze tena mtu kuona wanarefusha nyakati
za mpito wakizania kama nchi ina feza kwa hayo yote. Tamaa zao za uwezo
isiyoriziki imewapeleka kukubali «mpa-ngo wa 1+4 » unaojaa ndani
mwake chi-pukizi za ugonvi ku kichwa cha serkali ?.
Uzaifu wa Shirika la
kirahiya
9. Mwanzo
wa myaka 90, wakati Shirika la kirahiya ilijipatia matengenezo na kujiunda,
wakongomani walifurahi kama wamepata watu wakuweza kutetea na kukinga haki
zao. Kuwapo kwa hii shirika la kirahiya katika mambo ya siasa iliamsha
kitumaini kikubwa ndani ya watu. Wito wake usio wakisiasa uliiweka Shirika
hiyo kuwa chombo cha wanainchi wasiokuwa na tamaa ya siasa ao ya
kusharikia nayo. Tumetumainia kama itafanya kazi yake ya muunganisho ;
lakini, imejiachilia kuanguka katika fujo. Imegeuka ya kisiasa mpaka ikawa
zaifu sana na kuweka katika hatari sifa yake na mafaa za wanainchi.
10.
Migawanyo ndani mwake haifaidi kufikia mwisho wa fujo inayotawala
inchini. Zaidi ya kupigania uwezo unaowatambulisha wajumbe hawa,
miganyo kati yao na kutumiwa sawa vyombo na wengine hayo yote ni
hatari kubwa sana inayopunguza nguvu yao. Ijapokuwa kuna wanaume na
wanawake waaminifu, lakini kitendo chao kinasongwa sana na tamaa ya watu
wengi wenye kutafuta ukubwa.
Juu
ya mafaa ya mali na ya siasa, kuna mtu
9.
Mtu, « aliyeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu » (Mw 1,
26), ana bei kupita vitu vyote. Wito wake wa kimtu unamfanya kuwa mtu wa
Mungu na mwenye kustahili hesima kubwa sana. Katika JKK, heshima hiyo
imezarauliwa kwa ajili ya tamaa ya mali
isiyo na mipaka. Vita
zinazofwatana katika nchi yetu ni vita tu kwa ajili ya mali. Mali za
chini ya udongo ya Kongo imetamaniwa na wenyi nguvu wakitia moto wa
magonvi na mgawanyo kati ya wakongomani ili wapate namna ya kuchukua mali
hii. Kati ya wanaopata faida katika fujo hiyo wakifichama kuna wanainchi ;
wamojawao wametajiwa na ripoti ya ONU. Lakini kuna pia
hasa wageni wanaoiba na ufundi wote mali za Kongo
wao wenyewe ao wakipitia kwa watu wengine. Wanapata faida ndani ya
fujo hiyo na wanafanya namna yao yote ili fujo iendelee wapate kushota
mali, bila kuishurulikia rahiya iliyo na uwezo juu ya inchi na juu ya mali
ya inchi yake.
12.
Kwa hawa wote, tunasema kama juu
ya mali iliyo chini ya udongo inayotamaniwa
nao sana na yanayowaletea
taabu wakongomani, kuna watu ; inafaa kuheshimu ustahili na haki zao.
Lalamiko hilo lawaelekea hasa ndugu zetu wanaositasita kwa kujenga amani
sababu ya faida yao kuhusu siasa na mali. « Wenyi mali hawadumu »
(Zab. 49 [48] 13). Utajiri wa damu haumpe heshima mwenye mali na hauwezi
kuwa chemchemu ya raha (cf. Yob. 15, 29). Hivyo hivyo, kutawala kwa ujeuri
si kidemokrasia.
Hakuna kutetea mabadiriko ya mipaka ya JKK
11.
Hali ya siasa katika JKK inaonekana kuwa kitisho ao hatari ili nchi yenyewe isiwepo tena.
Mbele ya shuruli zote za kugawanya nchi vipandevipande, rahiya ya JKK
inakataa mambo haya kwa nguvu yake yote na kupigania umoja wa inchi. Kwa
jina la rahiya hiyo, tunaendelea kuhakikisha kwa nguvu yetu yote kama
umoja wa nchi na uhuru wa taifa havikubali muteteo wowote.
Ila tu njia ya amani inaweza kuokoa JKK
14.
Njia ya amani peke yake inaweza kutosha Kongo katika fujo, na taifa katika mateso na taabu. Ginsi alivyonena Baba Mtakatifu
Papa Yoano Paulo wa II wakati wa kusherehe siku ya amani ulimwenguni kote
kwa mwaka wa 2003 na ya ukumbusho wa myaka 4O wa barua “Amani duniani“
(Pacem in terris) ya Mwenyiheri Papa Yoano wa XXIII, hiyo amani -inayotamaniwa
sana katika nchi yetu- ina
nguzo nne: ukweli, uhaki, mapendo na
uhuru.
Wapigana vita na wafanya siasa wanapaswa
kujishurtisha kuimarisha nguzo hii nne kwa kuitosha inchi yetu katika hali
mbovu. “Kutamani amani si alama ya uzaifu, bali ya nguvu“.
15.
Kuchagua amani kwashurtisha
vitendo vya kuonekana. Hivyo, zaidi ya hotuba na matakio mema, ni lazima wapigana vita na wafanya siasa waonyeshe vitendo vya
amani wakiepuka ugonvi unaoleta bure vikwazo katika njia ya kufikia
amani. Taifa letu lingefurahi kama wapigana vita wangeweza kutenda
vitendo kamili vya amani, kwa mfano kuacha kabisa mapambano, kufanya ibada ya upatanyisho na
huruma, mzozo katika ukweli, kuruhusu watu watembee huru na vitu vipite popote
katika nchi ya JKK, kuvunja silaha ndogodogo mbele ya watu, na kazalika.
16.
Katika hali ya leo ya inchi yetu, njia ya amani yapita hasa kwa
heshima ya
makubaliano na kutimiza Mkataba uliotiliwa sahihi. Hakika
tumeonyesha uzaifu wa Mkataba wa jumla; ijapokuwa hiyo, tuaalika waliotia
sahihi juu yake waikamilishe ao waitimize katika yale yanoyoweza kusaidia
kuongoza inchi.
17.
Hakika, ijapokuwa uzaifu wa Mkataba wa jumla kuhusu mpito katika
JKK, Mkataba huo ni hatua ya lazima katika njia ya kufikia kwenyi
amani. Wajumbe katika Mkataba huo wanapashwa waziwazi kukataa vita na
ujeuri wowote unaosindikiza vita ; wote waweke silaha chini na kuanza
kazi ya kutengeneza jeshi iliyo kama mwanzo wa mpito usiokua
na chembe za ugonvi dani.
Mno ni mno !
18.
Uzidisho wa vikwazo katika njia ya kupata amani katika JKK umepita
kipimo cha uvumilivu wowote. Kufwatana na daraka zetu ndani ya taifa,
tunaarifu wapigana vita na wafanya siasa kama: rahiya
haitavumilia tena muda mrefu mizungukozunguko yao. Kama fujo inadumu,
Kanisa Katoliki litachukua mipango yakufaa
kwa kuharikisha amani katika JKK.
19.
Hali ya taabu wanayoishi watu wa Kongo haipashwe kuvunja mgongo
wakaaji wa Kongo.
Inatuita tujitambue sisi wote kwa kuharikisha ujio wa serekali
kamili. Kwa kufikia huko, sisi, Wachungaji na Baba zenu katika imani,
tunawaonya na kuwaalika ndugu na dada zetu wapigana vita pamoja na wafanya
siasa, waonyeshe utashi wa siasa na alama ya maadibisho ya kweli ya siasa.
Waache kupatisha Kongo haya na
wageuke viongozi vya kweli wa siasa.
20.
Tunawaomba wakristu wenyi kuwa katika Shirika la kirahiya wafanya
kweli kazi yao ya kuunganisha watu. Wawe mashuja wanaopigania mema kwa
kujenga inchi.
Baraka
ya mwisho
21. Kwa maombezi ya Bikira Maria Mtakatifu sana,
Malkia wa amani, Bwana abariki nchi yetu na amshe dani ya taifa letu
wajengaji wengi wa amani.
Imeandikwa
pale Kinshasa, tarehe 15
febrayo
2003
|